Ijumaa, 12 Desemba 2014

TIMU YA MAGEREZA (AFRICAN WANDERERS FC) KUCHUANA NA TIMU YA MKAMBA RANGERS YA MKOANI MOROGORO...



TIMU ya Magereza Iringa inatarajia kuchuana vikali na timu ya Mkamba Rangeres  ya  Kilombero, mkoani Morogoro, katika mechi itakayofanyika kesho, kwenye uwanja wa Samora.
Akizungumza na blog hii, Katibu wa timu ya Magereza (African Wonderers fc) ya mjini Iringa, Shukuru Steven alisema wanatarajia kuibuka na ushindi mnono katika ligi hiyo.

Alisema timu yake imejiandaa vyema kuingia kwenye mpambano huo, huku wachezaji wote wakiwa na afya njema.
“Hakuna majeruhi hata mmoja na tunatarajia kuibuka washindi katika mechi hiyo ya kesho tarehe 13,12/2014,” alisema Shukuru.


Shukuru amewataka wananchi wa Iringa kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa Samora ili kuishangilia timu yao.

HALI ILIVYOKUWA KATIKA UWANJA WA SOKOINE JIJINI MBEYA KATI YA AFRICAN WANDERERS NA WENDA FC

HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA JIJINI MBEYA


            KARIBU KWENYE BLOG YETU
KAZI ILIKUWA IKIKARIBIOA KUANZA...


KARIBUNI KWENYE BLOG YETU MPYA

KARIBU KWENYE BLOG YETU MPYA YA AFRICAN WANDERERS FC. TUTAKUWA TUKIWALETEA TAARIFA ZETU MBALI MBALI KUHUSU SOKA.